Proverbs 2:1-6

Faida Za Hekima


1 aMwanangu, kama utayakubali maneno yangu
na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,

2 bkutega sikio lako kwenye hekima
na kuweka moyo wako katika ufahamu,

3 cna kama ukiita busara
na kuita kwa sauti ufahamu,

4 dna kama utaitafuta kama fedha
na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,

5 endipo utakapoelewa kumcha Bwana
na kupata maarifa ya Mungu.

6 fKwa maana Bwana hutoa hekima,
na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
Copyright information for SwhKC