Proverbs 2:1-6
Faida Za Hekima
1 aMwanangu, kama utayakubali maneno yangu
na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
2 bkutega sikio lako kwenye hekima
na kuweka moyo wako katika ufahamu,
3 cna kama ukiita busara
na kuita kwa sauti ufahamu,
4 dna kama utaitafuta kama fedha
na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,
5 endipo utakapoelewa kumcha Bwana
na kupata maarifa ya Mungu.
6 fKwa maana Bwana hutoa hekima,
na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
Copyright information for
SwhKC